HUKUMU

 

FATAWA

 

       
       
       
       
Maskani Qurani Sunna Fiqhi Sera Tarehe Dua Masuala Fatawa Dunia
Uislamu Fatawa Fatawa Fatawa Fatawa Fatawa Fatawa Fatawa Fatawa Viungo

 

Fatawa: Hukumu za Sharia

اضغط هنا لعرض تفسير ابن كثير للآية

An Nahl 16:43 النحل  43:16
Nasi hatukuwatuma kabla yako ila wanaume tuliowateremshia Wahyi. Basi waulizeni wenye ukumbusho kama nyinyi hamjui

                         

Kitabu 25, Namba 3634 cha Abu Daud:

Book 25, Number 3634:

Amesimulia Abu Darda'a: Alisema Kathir ibn Qays kuwa: Nilikuwa nimekaa na Abu Darda'a ndani ya msikiti wa Damaskas, akamjia mtu na kumwambia: Abu Darda'a, nimekuja kwako kutoka Madina kwa Hadithi ambayo nimesikia kuwa umeisimulia kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW). Sikuja kwa madhumuni mengine yoyote yale.

Akasema: Nimemsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW) akisema: Mwenye kufuata njia kutafuta elimu,  Mwenyezi Mungu atamfanya afuate mojawapo ya njia za Peponi. Malaika watateremsha mbawa zao kwa furaha yao kubwa na yule mwenye kutafuta elimu, na wakaazi wa mbinguni na ardhini na samaki ndani ya maji watamuombea maghfira mwanachuoni. Fadhila ya mwanachuoni juu ya mcha Mungu ni kama ile ya mwezi, unapokuwa kamili, juu ya nyota zilizobakia. Wanachuoni ni warathi wa Manabii, na Manabii hawawachi dinari wala dirhamu, huwacha elimu tu, na yule mwenye kuichukuwa huwa amechukuwa fungu jingi.


                          Hadithi hii inatufahamisha umuhimu wa mtu kutafuta elimu hasa ile ya dini kwani dini ndio yenye kunadhimu maisha ya mtu hapa duniani na kumpatia cheo kikubwa kesho Akhera. Wanazuoni wana vyeo vikubwa mbele ya Mola wao na fadhila nyingi kabisa, na kwa sababu hii kila Muislamu anahimizwa kutafuta elimu popote ilipo ili aishi maisha yake akijua nini anachofanya, na aweze kuwaongoza wengineo awatoe kwenye giza la ujahili na kuwatia kwenye mwangaza wa elimu.

                          Kazi hii ya kuwaongoza wengine ni juu ya wanazuoni na maulamaa ambao Mwenyezi Mungu amewajaaliya kupata fursa ya kutafuta elimu ya dini na kujifunza Sharia yake na kujua lipi la halali na lipi la haramu, na ni juu ya watu hawa kuwaelimisha wenziwao na kuwatoa kwenye ujinga na kuwatia kwenye nuru ili waweze kushindana na kumpinga adui wao mkubwa Iblisi na makundi yake ya Mashetani katika wanadamu na katika majini.     

                           Hawa wanazuoni na maulamaa, baada ya kuzama katika bahari ya elimu na maarifa na kujua dini yao sawa sawa, hufikia mwisho daraja ya mufti, mtu ambaye mas-ala mbali mbali ya dini huwa na uwezo kutoa hukumu zake katika mambo tofauti tofauti ya maisha. Mufti hutowa fatawa juu ya mambo yanayohusu dini katika maisha ya Muislamu, na fatawa hizi huwa namna mbili: Kuna fatawa kuhusu hukumu mbali mbali za dini ambazo watu wa kawaida huwa hawazijui, na baada ya kuulizwa mwanachuoni mwenye elimu katika mas-ala haya, hutoa fatawa ambayo hutokana na ujuzi wake juu ya hilo jambo.

                            Fatawa nyengine huwa zinahusu mambo katika maisha ambayo Fiqhi au Sharia ya kiislamu haijagusia, katika mambo mapya yanayozuka katika maisha ya binadamu, kama hukumu zinazohusu benki, bima, kununua hisa za mashirika, na mambo menginewe mapya ya ulimwengu wetu wa leo. Fatawa kama hizi zinahitajia ujuzi wa elimu ya dini na kadhalika elimu ya lile jambo linaloulizwa, maana bila ya kuwa na ujuzi wa yote mawili mtu huweza akatoa fatawa za kimakosa na kuwapoteza wengine.  Kwa hivyo, inatakikana wanazuoni wachukuwe hadhari katika mambo kama haya.

                              Aidha, kuna fatawa ambazo zinahitajia kukutana maulamaa na wanazuoni wa ulimwengu wa kiislamu na kukubaliana juu ya hukumu ya jambo fulani katika maisha, na makubaliano haya huwa ni itifaki ya maulamaa na fatwa inayotoka huwa ni ijmaa ya umma na kwa hivyo, huwa ni fatwa madhubuti na hukumu ya sawa ya wanazuoni wote, na ijmaa ni mojawapo ya misingi ya dini ya Uislamu baada ya Qurani na Sunna za Mtume Muhammad (SAW).  

Nchi za kiislamu

Afghanistan

Albania

Algeria

Azerbaijan

Bahrain

Bangladesh

Benin

Brunei

Burkina Faso

Cameroon

Chad

Comoros

Djibouti

Egypt

Gambia

Guinea

G.-Bissau

Indonesia

Iran

Iraq

Jordan

Kazakhstan

Kuwait

Kyrgyzstan

Lebanon

Libya

Malaysia

Maldives

Mali

Mauritania

Morocco

Niger

Nigeria

 Oman

Pakistan

Palestine

Qatar

Saudi Arabia

Senegal

Sierra Leone

Somalia

Sudan

Syria

Tajikistan

Tunisia

 

Turkey

Turkmenistan

UAE

Uzbekistan

      Western Sahara

Yemen

 

Côte d'Ivoire

Ethiopia