SERA

 

MAISHA YA MTUME (SAW)

 

       
       
       
       
Maskani Qurani Sunna Fiqhi Sira Tarehe Dua Masuala Fatawa Dunia
Library Biography Muhammad Raheeq Message Timeline Brief Biography Proofs Viungo

 

Maisha ya Mtume Muhammad (SAW)

اضغط هنا لعرض تفسير ابن كثير للآية

Al Ahzaab 33:21 الأحزاب-: 21:33
Hakika nyinyi mnao mfano mwema kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa anayemtaraji Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, na akamkumbuka Mwenyezi Mungu sana

                  Baada ya Mwenyezi Mungu kuleta duniani Mitume na Manabii 123,999 kwa ajili ya kuwaongoza na kuwaelekeza njia ya sawa kaumu zao na watu wao mbali mbali, alimleta Mtume Muhammad (SAW) kuwa ndiye mwenye kukamilisha mfululizo huu wa wajumbe wa Mwenyezi Mungu kwa wanadamu, na akamfanya yeye kuwa ndiye wa mwisho na wa ulimwengu mzima na kwa wanadamu na majini wote.

                  Kwa hivyo, Mwenyezi Mungu Muumba wa viumbe vyote alimjaaliya Mtume Muhammad (SAW) kuwa ni kiumbe bora kabisa kuliko wote na kumpa kila sifa njema ambayo mwanadamu mkamilifu anatakiwa awe nayo ili aje kuwa ni mfano na kiigizo kwa wanadamu wengine duniani, na kwa ajili hii, Mtume (SAW) aliishi ulimwenguni akituonyesha mifano mbali mbali katika maisha na namna gani kuishi maisha kikamilifu kwa mujibu wa maelekezo na mafunzo ya mwenyewe Mola aliyetukuka.

                    Mtume Muhammad (SAW) baada ya kwisha kupewa utume alifundishwa kila lenye kheri na binadamu ili awafunze na kuwahimiza na kunabihishwa kila lenye shari na binadamu awazindue na kuwataka wajiepusha nalo ili maisha yao hapa duniani yawe ni mazuri, ya amani na furaha. Akawa yeye ndiye mwenye kuwaonyesha watu mifano hiyo, ili na wao wapate kuigiza na kuifuata.

                    Mtume, kwa hivyo, akaishi kama yatima, mtoto maskini mwenye kufanya kazi utotoni mwake, mvulana na barobaro mwenye kujua na kupigania haki, kijana mwenye kutafuta riziki yake ya halali kwa kufanya biashara kwa uaminifu na juhudi kubwa, mtu mzima mwenye kuaminiwa na watu wake kwa ukweli na uaminifu wake mpaka alipoteuliwa na Mwenyezi Mungu kuwa ni mjumbe wake na kuanza maisha mapya chini ya uwongozi na himaya ya Mola wake.

                      Baada ya kufikiwa na ujumbe kutoka kwa Mola wake na kuchaguliwa kuwa ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa watu wake na kwa umma wa kiislamu kwa jumla, maisha yake yaligeuka na kuwa ni mfano mzuri kwa wanadamu wote kwa jumla. Akawa ni kiongozi mwema na muadilifu, imamu wa waumini katika kumuabudu Mola wao, mwalimu mzuri wa kufundisha kila jema na kukataza kila ovu, mume mwema kwa wakeze na baba mzuri kwa wanawe na rahimu kwa watoto kwa jumla, jirani mwema kwa aliyekuwa Muislamu na asiyekuwa Muislamu, mtu karimu kwa maskini na mafakiri, sahibu mwema kwa wenzake na marafikize, kiongozi mzuri katika hali ya vita na hali ya amani

Nchi za kiislamu

Afghanistan

Albania

Algeria

Azerbaijan

Bahrain

Bangladesh

Benin

Brunei

Burkina Faso

Cameroon

Chad

Comoros

Djibouti

Egypt

Gambia

Guinea

G.-Bissau

Indonesia

Iran

Iraq

Jordan

Kazakhstan

Kuwait

Kyrgyzstan

Lebanon

Libya

Malaysia

Maldives

Mali

Mauritania

Morocco

Niger

Nigeria

 Oman

Pakistan

Palestine

Qatar

Saudi Arabia

Senegal

Sierra Leone

Somalia

Sudan

Syria

Tajikistan

Tunisia

 

Turkey

Turkmenistan

UAE

Uzbekistan

      Western Sahara

Yemen

 

Côte d'Ivoire

Ethiopia