QURANI

 

QURANI TUKUFU

 

       
       
       
       
Maskani Qurani Sunna Fiqhi Sera Tarehe Dua Masuala Fatawa Dunia
Uislamu Tafsiri Daraja Elimu Visomo Biblia Bishara Ushahidi Miujiza Viungo

 

Qurani:Wahyi wa Mwenyezi Mungu

اضغط هنا لعرض تفسير ابن كثير للآية

Al Israa:17:9 الإسراء: 17: 9

Hakika hii Qur'ani inaongoa kwenye ya yaliyo nyooka kabisa, na inawabashiria Waumini ambao wanatenda mema ya kwamba watapata malipo makubwa

                          Wahyi ni ujumbe wa Mwenyezi Mungu anaomteremshia mja wake aliyemchagua kuwa Nabii au Mtume kwa watu wake, kaumu yake au umma mzima. Tangu mwanzo, Mwenyezi Mungu alizungumza na Adam kwa njia ya Wahyi, na baada ya kumteremsha duniani akaendelea kupata Wahyi kama ni Nabii wa kwanza kwa watu wake. Baada yake, Manabii na Mitume wote waliokuja kuendeleza risala ya Mola wao hapa ulimwenguni walikuwa wakipata ujumbe huu kwa njia ya Jibril (AS) mmoja katika Malaika wakubwa kabisa na watukufu huko mbinguni.

                         Baada ya kufariki Adam (AS), Mwenyezi Mungu aliendelea kuteremsha Wahyi kwa Manabii na Mitume wengine kuwakumbusha wanadamu kuwa Yeye ndiye Mola wao aliyewaumba na kuwaleta ulimwenguni  na kuwaruzuku, na kuwazindua kuwa Iblisi ni adui wao na atafanya kila linalomkinika kuwapoteza na njia ya haki. Ujumbe huu uliendelea kuwateremkia hawa watu waliochaguliwa kuwaongoza wengine na kuwafikishia ukweli kupitia kaumu mbali mbali kama kaumu ya Nuhu, Ibrahim, Musa, Isa na wengineo.

                          Mtume Muhammad alikuwa wa mwisho katika mfululizo wa Manabii na Mitume hawa kupokea Wahyi na katika muda wa miaka ishirini na tatu aliteremshiwa Qurani Tukufu kwa ajili ya uwongofu wa mwanadamu wote kwa jumla kinyume na ujumbe wa Mitume iliyokuja kabla yake ambao ulikuwa ni ujumbe wa Mwenyezi Mungu kwa watu au kaumu fulani tu kama Wahyi alioteremshiwa Nabii Musa (Taurati), Nabii Daudi (Zaburi), na Nabii Isa (Injili) (rehema na amani ziwe juu yao).

                         Katika muda wa miaka 23 wakati Muhammad alipokuwa na miaka 40 mpaka alipofikia umri wa miaka 63, Qurani kwa njia ya Wahyi ilikuwa ikimteremkia Mtume (SAW) kutoka kwa Mola wake, na ujumbe huu ulikuwa umekusanya maamrisho na makatazo na maelekezo na simulizi mbali mbali za Umma zilizotangulia kwa ajili ya kuwaongoza Wanadamu duniani.

                        Ujumbe huu wa mwisho uliteremka kwa lugha ya Kiarabu kwa sababu Mtume Muhammad (SAW) alikuwa ni Mwarabu kama vile Taurati ilivyokuwa kwa Kiibria kwa Mtume Musa na Kiaramia kwa Mtume Isa. Hii ni kwa sababu wale watu wa mwanzo wanaopata ujumbe au risala hii waweze kufahamu madhumuni ya risala hii kutoka kwa Mola wao. Qurani imebakia mpaka leo katika lugha ile ile iliyoteremshiwa ya Kiarabu na watu wote ulimwenguni wanaisoma kwa lugha hii. Lakini wanaamrishwa watu wa mataifa na makabila mengine wajifunze Kiarabu na wafasiri hii Qurani kwa lugha zao ili waweze kufahamu zaidi maneno ya Mwenyezi Mungu. 

                         Qurani Tukufu ndio chanzo cha mwanzo cha Sharia ya Kiislamu, na kutokana na maandishi haya, Waislamu wanajifunza kila aina ya Ibada (Sala, Saumu, Zaka na Hija), na kila aina ya Maingiliano (ya kijamii, kisiasa, kiuchumi na kadhalika). Chanzo cha pili cha Sharia ni Sunna za Mtume Muhammad (SAW) na tofauti  baina ya Qurani na Sunnah ni kuwa Qurani ni Wahyi unaotoka kwa Mwenyezi Mungu na hakuna uwezekano wa kubadilika, na Sunna ni maneno, vitendo vya Mtume Muhammad katika muda wa utume wake, na yale ambayo yamefanywa katika uhai wake bila ya yeye kuyapinga au kuyatoa makosa na yanachukuliwa kuwa ni mambo aliyoyakubali kuendelewa kufanywa.

                         Leo Qurani baada ya miaka ya zaidi ya elfu na kitu ni yale yale maneno na maandishi yaliyoachwa na Mtume Muhammad kwa Waislamu, nayo husomwa na kuzungumzwa na kusomeshwa na kuhubiriwa na kufasiriwa na kufanyiwa uchunguzi mbali mbali na Waislamu na wasiokuwa Waislamu, na kila kukicha mambo mengi katika maisha na sayansi yanagunduliwa yakiwa yanakubaliana na yale yaliyokuwemo ndani ya hii Qurani.

Nchi za kiislamu

Afghanistan

Albania

Algeria

Azerbaijan

Bahrain

Bangladesh

Benin

Brunei

Burkina Faso

Cameroon

Chad

Comoros

Djibouti

Egypt

Gambia

Guinea

G.-Bissau

Indonesia

Iran

Iraq

Jordan

Kazakhstan

Kuwait

Kyrgyzstan

Lebanon

Libya

Malaysia

Maldives

Mali

Mauritania

Morocco

Niger

Nigeria

 Oman

Pakistan

Palestine

Qatar

Saudi Arabia

Senegal

Sierra Leone

Somalia

Sudan

Syria

Tajikistan

Tunisia

 

Turkey

Turkmenistan

UAE

Uzbekistan

      Western Sahara

Yemen

 

Côte d'Ivoire

Ethiopia